Kikongwe
aitwaye Asagwile Kihaka (78) mkazi wa Kata ya Ghana jijini Mbeya,
anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kubaka mwanafunzi wa
darasa la saba (12) (jina lina limehifadhiwa), katika shule ya msingi
Mbata jijini hapa.
Mtuhumiwa alitenda kosa hilo Desemba 14, mwaka uliopita nyumbani kwake
baada ya kumrubuni mtoto huyo kwa kumtuma aende kununua kuni za shilingi
1,000 na kuagiza ampelekee nyumbani kwake, ndipo alipochukua jukumu la
kumbaka mtoto huyo hadi kuzirai.
Binti
huyo ambaye mpaka sasa hajaweza kusema kwa kinywa hadi jumapili ya
Januari 8, mwaka huu ambapo alifanyiwa maombi katika kanisa la PHM
lililopo jijini hapa, ambapo aliweza kuzungumzia tatizo hilo kwa
maandishi na kudai kuwa mzee Kihaka ndiye aliyemtendea unyama huo.
Uchunguzi
uliofanywa na Hospitali ya wazazi Meta umebaini kuwa binti huyo mara
kadhaa amefikishwa hospitalini na kupatiwa matibabu ya homa, lakini
hakuzungumza kilicho msibu hadi pale aliupokuja kuandika kuwa kabakwa na
mzee huyo na kugundulika sehemu za siri zikiwa na michubuko na vidonda
hali ambayo ilithibitishwa kuwa kaingiliwa na mwanaume.
Hata
hivyo wananchi waliitisha mkutano wa hadhara kutokana na kuchoshwa na
vitendo vya Mzee Kihaka ambapo imetajwa kuwa ni tukio la tatu la mzee
huyo kutenda na viongozi wa Kata ya Ghana kumfumbia macho.
Mzee
Kihaka alikamatwa Januari 2, mwaka huu na kupelekwa Kituo cha Polisi
cha Kati cha Mkoa, ambapo Mtendaji wa Kata hiyo aliwasilisha barua ya
kumwekea dhamana hali iliyopingwa na wakazi na kuamua kuitisha mkutano
wa hadhara Januari 13 kwa hofu alikamatwa na kurudishwa mahabusu siku
moja kabla ya mkutano huo wa hadhara Januari 12.
Wakati
huohuo siku ya mkutano wa hadhara Diwani wa Kata hiyo Bwana Anjelo
Chavaligino hakuhudhuria mkutano huo hali iliyopelekea kuleta hasira kwa
wananchi hao na kisha kumtafuta hadi kumpata na kumleta kwenye mkutano
huku akizomewa na wananchi wengine walienda kupiga mawe vioo vya
nyumba ya Mzee Kihaka.
Mtandao huu umeshuhudia familia ya mzee huyo ikiangua kilio baada ya kunusurika na mawe hayo.
Jeshi
la polisi mkoani Mbeya lilifika eneo la tukio na kuzuia ghasia hizo na
Diwani wa kata hiyo Bwana Chavaligino ameahidi kuitisha mkutano ili
kujadili mstakabali wa Mzee Kihaka, huku kwa upande wao wananchi
wamemtaka Mzee huyo na familia yake kuhama eneo hilo.