Sunday, February 12, 2012

ASKOFU ASHINDWA NGUVU NA SHETANI AKIWA KANISANI

Nyoka amtoa baru mbunge


NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri, alitimua mbio kunusuru maisha yake na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).
Mwanri alikuwa mgeni rasmi kwa ajili ya kuendesha harambee ya kujenga Kanisa la Kilingi, akiwa na mkewe meza kuu, aliwashangaza waumini alipokimbia akiwa amenyanyua mikono juu huku akitamka maneno ya “shindwa kwa Jina la Yesu wewe shetani, shetani shindwa kwa Jina la Yesu,” na wageni wengine waalikwa wakianguka chini wakijiokoa. Hali hiyo ilitokea baada ya nyoka kutoka kusikojulikana kuingia kanisani huku Naibu Waziri akijiandaa kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa. Waumini walikimbizana na kiumbe huyo kwa mawe na viti bila kujali kama walikuwa ibadani, huku Askofu na wachungaji wengine wakiendelea kusali na waumini kutakiwa kurejesha utulivu katika ibada.
Tukio hilo lilitokea katika ibada ya saa nne iliyokuwa ikiongozwa na Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dk. Martin Shao, ambayo pia ilikuwa ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi huo.


Hata hivyo, jitihada za waumini za kumkimbiza nyoka huyo kutaka kumwua hazikufanikiwa, baada ya kutoweka asionekane tena, jambo lililoacha simulizi la ni kwa jinsi gani alifika mahali hapo.

“Inashangaza sana kwani lazima ujiulize alifikafikaje hapo mbele, wakati nyuma yangu kulikuwa na watu wengi...alikuwa na hasira sana, kwani alikuwa tayari kung'ata, kwa kweli hadi sasa mimi sielewi ni mambo gani haya,” alisema Mwanri.
  Hata hivyo hakuna madhara makubwa yaliyotokea mbali na mhamaniko uliowapata waumini hao. Nyoka huyo hakuweza kutambuliwa aina yake kutokana na mtafaruku
   

AUAWA KISHA MWILI WAKE KUCHARANGWA KAMA MNYAMA AKIWA KILABUNI







MBOZI
NI tukio la kusikitisha na kuleta simanzi ambalo limetokea katika familia ya Mzee Jackson Mwashiuya(78) na wakazi wa  mtaa wa Ichenjezya mjini Vwawa wilayani Mbozi mkoani Mbeya baada ya mjukuu wake Dominick Mwashiuya kutekwa na watu wasiofahamika kisha kumuua kikatili kwa kukatwakatwa viungo vyake vya mwili na kutelekezwa katika chumba cha kuuzia pombe za kienyeji.
 
Tukio hiolo la Mauaji ya kusikitisha limetokea Ijumaa majira ya saa 11 jioni ambapo marehemu aliitwa na mmoja wa wanawake wanaouza pombe ya Ulanzi katika kilabu maarufu ya pombe za kienyeji inayofahamika kwa jina la ’Kwa Jimmy’ambapo muda mfupi baadaye marehemu alikutwa akiwa amekufa huku mwili wake ukiwa umetapakaa damu.
 
Mwili huo wa marehemu ulikutwa katika chumba kilichoandikwa ‘Ikumbilo Kilabu’ ambapo muuzaji wa chumba hicho mwanamke aliyefahamika kwa jina moja la Nampashi alitoweka na watu wasiofahamika wanaodaiwa kuhusika na mauaji hayo.
 
Babu wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Mzee Jackson Mwashiuya alisema kuwa,  majira ya saa 11 jioni alikutana na mwanaye aliyefahamika kwa jina la Maria ambapo muda mfupi baadaye marehemu ambaye ni mjukuu wake wa mtoto wa kiume alikuja kwa ajili ya  kumsalimia shangazi yake.
 
Mzee Mwashiuya alisema kuwa wakati mjukuu wake akisalimiana na shangazi yake mara alifika mwanamke anayeuza ulanzi katika chumba kilichoandikwa ‘Ikumbilo Kilabu’ anayefahamika kwa jina moja la Nampashi ambaye alimuita marehemu na kwenda naye katika chumba anachouzia pombe aina ya ulanzi.
 
 
Alisema kuwa yeye aliondoka na kuingia katika chumba kingine kilichopo Kilabuni hapo ambapo alijumuika na watu wengine katika burudani ya kunywa pombe za kienyeji bila kujua kinachoendelea katika chumba cha pili ambacho kimepakana na chumba walichokuwa wameketi wao.
 
‘’Sikujua kinachoendelea katika chumba cha pili nilikaa na wazee wenzangu tunakunywa komoni, baadaye walifika watu kutueleza kuwa kuna mtu ameumizwa chumba cha pili…wote tulitoka ndani na kusimama nje ya chumba alichofia marehemu bila kujua ni nani aliyemo humo ndani,’’alisema Mzee Mwashiuya.
 
Alisema kuwa walichungulia katika chumba hicho na kuona miguu na damu ikiwa inachuruzika na kwamba kwa kuwa chumba kilikuwa na giza hawakuweza kuutambua vyema mwili wa marehemu kwa wakati huo.
Akizungumzia tukio hilo Mwenyekiti wa mtaa wa Ipanga ambao umepakana na mtaa wa Mpakani lilipotokea tukio Bw.Joseph Lwenje alisema kuwa mara baada ya kupata taarifa za tukio hilo aliingia katika chumba hicho na kumulika kwa kurunzi ambapo alikutana na dimbwi la damu huku mwili wa marehemu ukiwa na majeraha makubwa.
 
Alisema kuwa alitoa taarifa kwa Ofisa Mtendaji wa mtaa wa Bw.Tuliani Mwahalende ambaye aliondoka pamoja na mmoja wa wazee wa kamati ya  ulinzi na usalama ya mtaa huo Bw.Herman Mpinga hadi kituo cha Polisi na kutoa taarifa za tukio hilo na  askari polisi walifika eneo hilo na kuukagua mwili wa marehemu ndipo ilipofahamika kuwa aliyeuawa ni mjukuu wa Mzee Mwashiuya.
 
Kwa upande wake baba wa marehemu Bw.Richard Mwashiuya alisema kuwa alifika eneo la tukio muda mfupi mara baada ya kusikia minong’ono ya kuwepo mtu ndani ya chumba alichofia lakini hakujua kama aliyeuawa kuwa ni mwanaye ambaye ni mtoto wa kwanza kati ya watoto wake sita.
 
Alisema kuwa mara baada  ya kutokea mauaji hayo kumeibuka tetesi kuwa  kijana wake alikuwa akishiriki mapenzi na mwanamke anayeuza pombe za kienyeji ambapo pia inadaiwa kuwa mwanamke huyo alikuwa na mwanaume mwingine ambaye pia alikuwa akihusiana naye kimapenzi.
 
Baba mzazi wa marehemu alisema kuwa walishiriki katika kuukagua mwili wa marehemu katika hospitali ya wilaya ya Vwawa ulikohifadhiwa na kubaini majeraha makubwa ya kukatwa na kitu chenye ncha kali ambapo viganja vya mikono yake na vidole viliachana huku sehemu ya fuvu lake la kichwa ikiwa imefumuka kiasi cha kuonekana ubongo.
 
Alisema mazishi ya kijana wake yalifanyika katika makaburi ya Isangu yaliyopo Vwawa wilayani Mbozi majira ya saa tisa alasiri.
 
Aidha kufuatia mauaji hayo kamati ya ulinzi ya mitaa miwili ya Mpakani na Ipanga ilikusanyika kujadili tukio hilo na kufikia uamuzi wa kufunga Kilabu hicho cha pombe za kienyeji kutokana na kuonekana kuwa eneo hilo limekuwa ni chanzo cha uhalifu.
 
Akizungumzia kufungwa kwa Kilabu hicho Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa wa Mpakani Bw.Danford Mhema alisema kuwa kamati ya ulinzi na usalama ya mtaa iliketi na kujadili na hatimaye kugundua kuwa Kilabu hicho mbali na kuuza pombe za kienyeji ni danguro la ngono na uvutaji wa dawa za kulevya ambalo pia linaficha wahalifu.
 
Alisema kuwa eneo hilo pia ni maarufu kwa uchezaji wa kamari ambapo pia Kilabu hicho kinakesha hadi usiku wa manane jambo ambalo limekuwa kero kwa wakazi wa maeneo hayo huku mmiliki wa eneo hilo Bw.Jimmy Mwamlima akishindwa kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyofanyika katika Kilabu chake.
 
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na linafanya uchunguzi kuwanasa wauaji ili kuwafikisha mikononi mwa sheria.
 

Friday, January 27, 2012

RAIS WA MBEYA BROADCASTERS NETWORK APATA MTOTO

 MTOTO WA KWANZA WA RAIS WA MBN JINA LAKE NI CATHERINE MBWILE

 GABRIEL MBWILE AKITABASAMU NYUMBANI KWAKE NA MKEWE MAENEO YA AIRPORT JIJINI MBEYA



SHEMEJI MTU NAYE HAKUKOSA KUJA KUMUONA KICHANGA HUYO NA KUMTUNZA KWA VITU MBALIMBALI

Sunday, January 15, 2012

MAELFU WAOMBOLEZA KIFO CHA REGIA

 Rais Jakaya Kikwete akijiunga na waombolezaji katika msiba wa Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Mh Regia Mtema leo January 15, 2012 nyumbani kwa marehemu Tabata jijini Dar es salaam ambako Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda, Spika Anne Makinda na Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe walikuwapo.

 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa Chama Cha CHADEMA Mh Freeman Mbowe wa tatu kutoka kulia pamoja na jamaa wa Marehemu Regia Mtema.
Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katikati pamoja na Spika wa Bunge Mh. Anne Makinda.

PICHA NA IKULU YA TANZANIA

BAN KI MOON AMUONYA ASSAD

DW
Miezi  kumi  baada   ya  ghasia   kuzuka  nchini  Syria , katibu  mkuu  wa  umoja  wa  mataifa  Ban Ki-moon ametaka   rais  wa  Syria  Bashar al-Assad  kuacha kuwauwa  watu  wake.
Ban  alikuwa  akizungumza  katika  mkutano  mjini  Beirut kuhusu  demokrasia   katika  mataifa  ya  Kiarabu. Wakati huo  huo , Assad  ametangaza  msamaha  kwa  makosa yaliyofanywa  wakati  wa  machafuko  nchini  humo. Hatua hiyo  inahusu  pia  ukiukaji  wa  sheria  katika maandamano  ya  amani , kuwa  na  silaha  kinyume  na sheria  na  kulikimbia  jeshi. Kuachiliwa  kwa   wafungwa  ni moja  kati  ya  masharti  muhimu   ya  mpango  wa  mataifa ya  Kiarabu  ulioidhinishwa  na  Syria  hapo  Novemba mwaka  jana  kumaliza  mzozo  wa  nchi  hiyo, ambao umoja  wa  mataifa  unakadiria  kuwa  umesababisha  watu 5,000  kupoteza  maisha  yao. Jana  Jumapili ,  kiasi  ya watu  21  wameuwawa.

IKULU YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA CHADEMA KUFUATIA KIFO CHA MHESHIMIWA REGIA MTEMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mheshimiwa Freeman Mbowe, kuomboleza kifo cha Mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho, Mheshimiwa Regina Mtema.

Mheshimiwa Mtema ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Waziri Kivuli wa Kazi na Ajira amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Ruvu, Mkoa wa Pwani, asubuhi ya leo Jumamosi, Januari 14, 2012.

Katika salamu zake, Mheshimiwa Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Mbowe kuwa amesikitishwa na kuhuzunishwa na habari za kifo cha mbunge huyo ambaye amepoteza maisha akiwa bado kijana na kwamba pigo hilo siyo kwa Chama cha Chadema peke yake bali ni kwa taifa zima.

“Nimepokea kwa masikitiko na huzuni nyingi habari za kifo cha Mheshimiwa Mtema katika ajali ya gari. Siyo kwamba ajali hii imechukua maisha ya kijana bali imelinyang’anya taifa mbunge hodari, na kwa hakika, kifo chake siyo tu ni pigo kwa chama chako cha CHADEMA bali ni pigo kwa sote na kwa taifa letu kwa jumla. Nakutumia wewe binafsi, chama chako na wanachama wake salamu za dhati ya moyo wangu kuomboleza kifo na msiba huu mkubwa.”

“Napenda ujue kuwa niko nanyi katika msiba huu. Napenda vile vile uniwasilishie salamu zangu za rambirambi za dhati kabisa kwa wana-familia, ndugu na jamaa wa marehemu Mheshimiwa Mtema. Wajulishe kuwa nimepokea habari hizo kwa uchungu mwingi na kuwa moyo wangu uko nao katika wakati huu mgumu wa maombolezo, “ amesema Mheshimiwa Rais na kuongeza.

“Aidha, wajulishe kuwa nawaombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, awajalie uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu kwa sababu yote ni mapenzi yake. Naungana nawe, Mheshimiwa Mwenyekiti, na wanafamilia wa marehemu kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke pema peponi roho ya Mheshimiwa Regina Mtema. Amen.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu,
DAR ES SALAAM.

14 Januari, 2012




MELI YAPINDUKA


DW

Nahodha wa meli ya abiria atiwa korokoroni nchini Italia ,huku uchunguzi ukifanyika juu ya madai ya kuuwa bila kukusudia.

Vyombo  vya  habari  nchini  Italia  vimeripoti   jana  kuwa nahodha  wa  meli  ya  abiria ,inayojulikana  kama  Costa Concordia , ambayo ilipinduka katika  pwani  ya  Toscana , nchini  Italia, ikiwa  na  abiria  4,000  amekamatwa  wakati uchunguzi   unafanyika  juu  ya  madai   ya  kuuwa  bila kukusudia  na  kuitelekeza  meli  yake. 

 

Meli  hiyo  ya  abiria  iligonga  mwamba  baharini  na kusababisha  tundu  la  mita  70  hadi  100  katika  eneo lake  la  mbele , muda  mfupi  baada  ya  kuanza  safari siku  ya  Ijumaa  kutoka   bandari  ya  Civitavecchia  karibu na   Rome. 
Kiasi  ya   watu  42  wamejeruhiwa ,  ambao watu  wawili   hali  zao  ni  mbaya  na  wengine  41  ambao ni  miongoni  mwa  watu  waliokuwa  ndani  ya  meli  hiyo wakiwa  hawajulikani  waliko. 
Meli  hiyo  ilikuwa  ikielekea katika  bandari  ya  Savona  kaskazini-magharibi  ya  Italia na  ilitarajiwa  kusimama  katika  bandari  za  Marseille nchini  Ufaransa  pamoja  na  Barcelona  nchini  Hispania.