DW
Miezi kumi baada ya ghasia kuzuka nchini Syria ,
katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon
ametaka rais wa Syria Bashar al-Assad kuacha
kuwauwa watu wake.
Ban alikuwa akizungumza katika mkutano mjini Beirut
kuhusu demokrasia katika mataifa ya Kiarabu. Wakati
huo huo , Assad ametangaza msamaha kwa makosa
yaliyofanywa wakati wa machafuko nchini humo. Hatua
hiyo inahusu pia ukiukaji wa sheria katika
maandamano ya amani , kuwa na silaha kinyume na
sheria na kulikimbia jeshi. Kuachiliwa kwa wafungwa ni
moja kati ya masharti muhimu ya mpango wa mataifa
ya Kiarabu ulioidhinishwa na Syria hapo Novemba
mwaka jana kumaliza mzozo wa nchi hiyo, ambao
umoja wa mataifa unakadiria kuwa umesababisha watu
5,000 kupoteza maisha yao. Jana Jumapili , kiasi ya
watu 21 wameuwawa.
No comments:
Post a Comment