Wahamiaji 20 Wasomali walipatikana wamekufa wiki
iliyopita mashariki mwa Tanzania. Duru za polisi zimeeleza
jana kuwa huenda walitupwa kichakani kutoka kwenye lori
la mfanyabiashara magendo baada ya kukosa hewa ya
kutosha na kufariki.
Kamanda wa jeshi la polisi wa mkoa
wa Morogoro, Adolphina Chialo amesema wanafanya
uchunguzi na kisha hicho na watatoa taarifa baadaye,
lakini miongoni mwa waliouwawa ni wanawake watatu.
Polisi wamesema wahamiaji hao wanadhaniwa walikuwa
njiani kwenda Zambia au Afrika Kusini na walipatikana
katika sehemu tofauti kando ya barabara kati ya Desemba
26 mwaka jana na Januari mosi mwaka huu. Maelfu ya
Wasomali huikimbia nchi yao iliyokabiliwa na baa la njaa
kila mwezi, baadhi wakielekea kambi za wakimbizi katika
nchi jirani za Kenya na Ethiopia na wengine kwenda
kutafuta ajira katika mataifa mengine kupitia msaada wa
wafanyabiashara wa magendo.
No comments:
Post a Comment