MTOTO Oscar Oliver (17)
mkazi wa Ilemi Jijini Mbeya amechomwa kiganja chake cha mkono wa kushoto na kaa
la moto kwa kulazimishwa na mjomba wake akituhumiwa kuwa hana tabia njema.
Tukio
hilo la kinyama
limetokea usiku wa kuamkia siku ya sikukuu ya Krismas nyumbani kwa Andendekisye
Mwakabubu (30) ambaye ndiye anayedaiwa kufanya unyama huo kwa mpwa wake
akimtuhumu kuwa alitaka kumwibia.
Mwakabubu
anadaiwa kumlazimisha mtoto huyo kushika kaa la moto na baada ya mtoto huyo
kuungua kiganja chake alimpeleka katika kituo kidogo cha polisi cha Mwanjelwa
na kumfunmgulia kesi ya wizi wa kuibiwa vitu mbalimbali ili kuweza kuficha
unyama wake huo.
Baada
ya kufungua kesi hiyo, askari polisi walimshikilia kijana huyo na kumpeleka
katika kituo kikuu cha polisi mkoani hapa na kumweleza mlalamikaji huyo bandia
kuwa alitakiwa kufika kituoni hapo kwa ajili ya mtoto huyo kupelekwa
mahakamani.
Mtoto
huyo alipofikishwa katika kituo hicho kikuu alikutana na askari waliopo ndani
ya kitengo cha kuelimisha jamii kuhusu unyanyasaji wa kijinsi hususani kwa
watoto ambao walimsikiliza mtoto huyo na hatimaye jana walimwita mpwa wake kwa
ajili ya kutoa maelezo.
Mwakabubu
baada ya kufika kituoni hapo na kutoa maelezo na kuulizwa kuwa nani aliyehusika
na tukio hilo
alishindwa kubainisha huku akisema kuwa hajui aliyemchoma huku akisahau kuwa
katika maelezo yake ya awali yeye ndiye alikuwa mlalamikaji jambo ambalo
liliwashawishi askari hao kumakamata na kumpeleka rumande.
Mpwa
huyo wa mtoto Oscar akiwa mahabausu ya kituo hicho cha polisi, askari hao
wanaunda mtandao huo wa kuelimisha jamii juu ya unyanyasaji wa kijinsia mkoani
hapa hususani kwa watoto walimchukua mtoto huyo na kumpeleka Hospitalini kwa
ajili ya matibabu.
Mwakabubu
alihojiwa na askari wa mtandao huo wakiongozwa na askari aliyefahamika kwa jina
la Pudensiana Baito huku mwandishi wa habari hizi akiwa anafuatilia tukio hilo
na askari huyo alipotakiwa kueleza kwa undani tukio hilo alisema kuwa yeye si
msemaji wa jeshi la polisi.
No comments:
Post a Comment