Kiongozi mpya wa Korea Kaskazini anaongoza msafara wa
mazishi ya baba yake Kim Jong Il, ambao unapita katika
mitaa ya mji mkuu wa Pyongyang uliofunikwa na barafu na
theluji. Picha za Televisheni ya taifa ya Korea Kaskazini
zimemuonyesha Kim Jong Un akitembea sambamba na
gari lililobeba jeneza la baba yake.
Gari jingine lililobeba picha kubwa ya hayati Kim Jong Il
lilifuatia katika msafara huo. Maelfu ya waombolezaji
wamejipanga kando kando ya barabara wakivumilia baridi
kali kumuaga kiongozi wao, na wanajeshi wanainamisha
vichwa vyao kutoa heshima.
Kim Jong Il alikufa kutokana na mshituko wa moyo mapema
mwezi huu, na mazishi yake yatachukua muda wa siku
mbili. Mara tu baada ya kifo chake, vyombo vya habari
viliashiria kwamba Kim Jong Un ndiye atakayerithi
madaraka ya baba yake.
No comments:
Post a Comment