Thursday, December 22, 2011

ZAIDI YA WATU 50 WAUAWA NCHINI IRAQ

DW
Huku viongozi wa kisiasa wa Iraq wakiwa katika mgogoro wa kimadaraka na kisheria, inaonekana vurugu zinazotokana na madhehebu zimeanza tena nchini humo, baada ya makumi ya watu kuuawa hivi leo katika miripuko ya mabomu. 

Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani ya Iraq, jumla ya mashambulizi 11 yanayoonekana kupangwa vyema, yamewauawa kwa uchache watu 50 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 170. Mashambulizi hayo yamefanywa asubuhi ya leo wakati watu wakikimbilia kazini katika kila kona ya mji mkuu, Baghdad.

 

Maafisa wa usalama wamesema maeneo yaliyoshambuliwa ni Allawi, Bab al-Muatham na Karrada yaliyo katikati ya Baghdad, Adhamiyah, Shuala na Shaab yaliyo upande wa kaskazini, Jadriyah upande wa mashariki, Ghazaliyah upande wa magharibi na Al-Amil na Dura kwa upande wa kusini.


Mauaji haya yamefanyika katika wakati wanasiasa nchini Iraq wakilumbana juu ya hati ya kukamatwa kwa makamo wa rais, Tariq al-Hashimi, ambapo Waziri Mkuu Nouri al-Maliki ameitaka mamlaka ya jimbo la Kurdi, kumkabidhi kiongozi huyo wa Kisunni kwa serikali yake, kukabiliana na mashitaka ya kupanga mashambulizi dhidi ya viongozi wa serikali.

 

No comments:

Post a Comment