Watu wanne wamepoteza maisha katika matukio mawili
tofauti mkoani Mbeya likiwemo la mwanaume mmoja kuuawa kwa kutuhumiwa kufanya
mapenzi na mke wa mtu.
Jeshi la Polisi mkoani
humo limesema tukio la kwanza limetokea
Jumatatu ya Desemba 26, mkazi wa Kabwe jijini Mbeya aliyefahamika kwa
jina la Theresia Mbinili (85) alipoteza maisha baada ya gari namba T. 429 AHU
aina ya Toyota Hiace kumgonga.
Taarifa hiyo imesema kondakta wa gari hilo Joshua Laudeni (25)
mkazi wa Iyunga amekamatwa na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya, na chanzo
cha ajali hiyo ni kondakta huyo
kutosomea udereva na kuendesha bila leseni.
Tukio la pili limetokea
Jumatatu ya Desemba 26, mkazi wa Ilongo wilayani Mbarali aliyefahamika kwa jina
la Mbatalile Mwakilolile (70) kufa kwa kugongwa na gari namba T 881 BTT aina ya
Toyota Hiace katika barabara ya Mbeya-Iringa.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na Jeshi hilo imesema gari hilo lilikuwa
likiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina moja tu la Sunday, ambaye alikimbia
baada ya tukio.
Pia imesema mwili wa
marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Chimala Mission na kwamba chanzo cha
ajali hiyo ni mwendo kasi.
Jeshi la Polisi mkoani
Mbeya limeongeza kusema, mkazi wa Ifuko wilayani Chunya aliyefahamika kwa jina la
Zaina Zawadi (55) amefariki wakati akipatiwa matibabu katika Kituo cha Afya cha
Mbuyuni baada ya kupigwa na mwanamke mwenzake.
Imebainika aliyempiga hadi
kusababisha kifo chake ni Justa Stephen ambaye amekimbia baada ya kutenda kosa hilo, akimtuhumu marehemu kwa imani za ushirikina na anatafutwa na Jeshi hilo kwa hatua zaidi.
Katika hatua nyingine
Jeshi hilo limesema mwanaume mkazi wa
Chipaka wilayani Mbozi aliyefahamika kwa jina la Amos Siame (37) ameuawa kwa
kukatwa na vitu vyenye ncha kali kisha kunyongwa kwa kamba ya gome la mti na
kutupwa porini karibu na makaburi ya Chipaka.
Kwa mujibu wa Taarifa kwa
vyombo vya habari kuhusu tukio hilo
iliyotolewa imesema mwili wa marehemu
umekutwa na jeraha kubwa shingoni.
Pia imeongeza kusema
chanzo cha mauaji hayo ni marehemu kutuhumiwa kufanya mapenzi na mke Jacob
Sikaonya (31) mkazi wa Chipaka.
Aidha watu watano
wanashikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo akiwemo
Frank Sikaonya (28), Nimrodi Sikaonya, Waikunga Sikaonya na Ayub
Sikaonya (18).
Imeandikwa na Rester Phares Redio
Ushindi FM Mbeya Tanzania Desemba 27, 2011.
No comments:
Post a Comment