Saturday, December 31, 2011

WAKRISTO WATAKIWA KUWA NA MIPANGO KWA AJILI YA MWAKA 2012

Wakristo mkoani Mbeya wametakiwa kuwa na mipango kwa maisha yao ya  baadaye badala ya kutegemea kudra za Mwenyezi katika mafanikio yao.
Akizungumza katika Ijumaa ya Marafiki Meneja wa Benki ya Stanbic Tawi la Mbeya Willy Afumwisye amesema wakristo wengi wamekosa mipango katika maisha yao licha ya Neno la Mungu kuwapa ahadi kedekede.

Pia amesema wakristo wengi wamekuwa wakitegemea kuwekewa mikono na Watumishi wa Bwana ili waweze kufanikiwa kitu ambacho wakati mwingine sio sahihi isipokuwa ni uzembe wa kiakili.

Hata hivyo amesema kumtanguliza Mungu katika kila jambo ni muhimu sana kwani hakuna mafanikio bila Muumba wa Mbingu na Nchi na kuongeza kuwa anapopanga ni lazima kupanga na Roho Mtakatifu.

FOF Jijini Mbeya ni ya Pili, hufanyika kia Ijumaa ya mwisho wa mwezi. Washiriki akali ya 35 walikuwepo katika Ijumaa ya Marafiki Jijini Mbeya.

Imeandikwa na Johnson Jabir Redio Ushindi FM Desemba 30, 2011.

No comments:

Post a Comment