Wednesday, December 28, 2011

KUPANDA BEI MAFUTA JIJINI MBEYA KWAIBUKWA MZOZO


Mzozo umeibuka Jijini Mbeya baina ya madereva wa magari na wamiliki wa vituo vya mafuta kufuatia wamiliki hao kuzuia mafuta kuuzwa katika vituo vyao kwa siku ya pili sasa.

Uchunguzi uliofanywa na redio Ushindi FM umebaini foleni kubwa katika baadhi ya vituo vya mafuta Jijini Mbeya  kwa magari hayo kutaka nishati hiyo.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyobainishwa na Redio hiyo yamebaini Kituo cha Mafuta cha JM kilichopo Maghorofani Jijini humo foleni kubwa ya magari hali ambayo imekuwa tofauti na siku nyingine.

Madereva wa magari hao wamenukuriwa wakisema mrundikano huo umetokana na EWURA kutangaza bei mpya za nishati hiyo, na kuongeza kuwa wanaiomba serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwachukulia hatua stahili wamiliki hao kwani wanachangia kukwamisha shughuli za kimaendeleo nchini.

Wamiliki wa vitu hivyo kwa upande wao wameishutumu Mamlaka husika kutokana na kushusha bei hali ambayo imewaongezea  hasara na kuongeza kuwa awali ilikuwa shilingi 2,200 na sasa ni shilingi 1,800

EWURA huwa na kawaida kila baada ya majuma mawili kubadilisha bei elekezi ya nishati hiyo kwa kila wilaya nchini Tanzania kufuatana na umbali kutoka hazina hadi kwa mteja.

*  Bei za nishati ya mafuta katika mkoa wa Mbeya kwa ujumla tangu Desemba 19, 2011

PETROL
DIESEL
KEROSENE
MBEYA
1989
2082
2065
CHUNYA
1999
2092
2074
ILEJE
2002
2096
2078
KYELA
2005
2098
2081
MBARALI
1973
2067
2049
MBOZI
1998
2092
2074
RUNGWE
1998
2091
2074

*Bei hizi zimeanza kutumika Jumatatu ya Desemba 19, 2011
      
            
Moses Mbembela na Rester Pharles Redio  Ushindi FM Desemba 28, 2011

No comments:

Post a Comment